BEEF ROAST

BEEF ROAST
Mahitaji :

Nyama ya Ng'ombe ya kawaida kilo 1 iliyochemshwa na kuiva.
Vitunguu maji vilivyokatwakatwa 2
Kitunguu swaumu 1/2 kjk cha chai
Tangawizi 1/2 kjk cha chai
Nyanya zilizokatwakatwa 15
Viazi mviringo vilivyokaangwa 10
Curry powder kjk 1 cha chai
Garam masala kjk 1 cha chai
Mdalasini wa unga kjk 1 cha chai
Pilipili ya unga 1/2 kjk cha chai
Chumvi kiasi chako
Mafuta ya kupikia kiasi
Majani ya giligilani 1/2 fungu

Maelezo :

Bandika chombo na weka mafuta.. yakipata moto weka Vitunguu maji kaanga mpaka vikikaribia kufikia kua rangi ya dhahabu weka tangawizi na kitunguu swaumu na curry powder,garam masala,mdalasini wa unga,pilipili ya unga.
Kaanga kwa dakika 1. Kisha weka nyanya na nyama na Viazi na chumvi...kaanga mpaka nyanya zilainike kidogo. Wakati unakaanga kama roast linakaukia utaweka supu kidogo kidogo.
Endelea kukaanga mpaka nyanya zinalainika kabisa na mafuta yanajitokeza.
Inategemea na uzito wa roast unaotaka.
Mwagia majani ya giligilani kwa juu.

Baada ya hapo roast tayari kuliwa na chapati.

No comments:

Post a Comment