KATLES ZA SAMAKI


Mahitaji:

viazi kiasi 1/2 kilo
Samaki 1
mdalasini wa unga kijiko cha chai 1
Binzari nyembamba kijiko 1 itwange
Majani ya Kotmir fungu 1
Kitunguu swaum kilichopondwa kijiko 1 cha chai
Kitunguu maji 1 katakata
Ndimu 1
Chumvi kiasi
Pilipili manga 1/2 cha chai
Binzari manjano kijiko 1 cha chai
Mafuta ya kupikia kiasi
Chenga za mkate kiasi
Mayai 2 yaliyopigw kabisa

JINSI YA KUPIKA  :

1.Chemsha samaki mtie,swaum mdalasini,binzari nyemba,chumvi,manjano ,pilipili manga na ndimu na maji kidogo kama robo kikombe tu.mchemshe akaukie kisha mtoe miba yote halafu mvuruge achanganyike vizuri na viungo

2.Chemsha viazi na maji kiasi  ,vitie chumvi,vitunguu maji na kotmir na thoum kidogo vikiiva tu vichuje maji kisha viponde ponde vizuri kisha tia ule mchanganyiko wa samaki halafu tengeneza shepu ya katlesi upendayo

3.Chovya katika chenga za mkate kisha chovya katika yai kisha kaanga katika mafuta lkn mafuta yawe kidogo yasifunike katles, kaanga zikiwa brown toa zichuje mafuta.katles tayari kuliwa na chatne yoyote upendayo

No comments:

Post a Comment