SIMPLE CAKE :

SIMPLE CAKE :

Siagi kikombe 1
Sukari kikombe 1
Mayai 4
Baking powder kijiko cha chai 1
Unga wa ngano kikombe 1 na nusu
Vanilla kijiko 1 cha chai

JINSI YA KUANDAA.

1.Kwenye bakuli tia Unga wa ngano na baking powder changanya vizuri kwa kijiko weka pembeni

2.Washa oven  180c kama unapikia mkaa koleza jiko kabisa.

3.Saga siagi na sukari mpaka iwe laini, tia yai moja moja huku uwe unasaga vizuri mpaka mayai yamalizike  , tia vanila changanya tena vizuri,

4.Tia unga wa ngano , saga  kidogo tu malizia kukoroga na mwiko.
Paka mafuta kwenye trey chini ili cake isigande , tia mchanganyiko wako ueneze vizuri na ubake mpaka iwive, ichome na kijiti, kujiti kikitoka  kikavu cake imewiva itoe, iwache ipoe kwa dakika 10 mpaka 15.
Kama unapikia kwenye mkaa weka moto juu na chini kama moto wa kupalilia wali.

5.Ikate kate vipande saiz unayotaka,kula na juice,chai n.k ENJOY. IMETUMIKA MEASURING CUP KWAJILI YA KUPIMIA VIPIMO NA HAIJATIWA MAZIWA!

No comments:

Post a Comment