FISH FINGER :SAMAKI


      FISH FINGER (SAMAKI)

MAHITAJI :A:
💎Unga wa ngano vijiko vikubwa 3
💎Kitunguu thoum kijiko 1
💎Binzari manjano kijiko 1
💎Curry powder kijiko
 1
💎Pilipili manga 1/2 kijiko
💎Pilipili ya unga kijiko1
💎Chumvi kiasi chako
💎Tangawizi iliyopondwa kijiko 1
💎mayai 2

MAHITAJI :B:

💎Samaki (mnofu) vipande 3 vikubwa,katakata vipande virefu virefu kama katika picha inavyoonesha.
💎Mafuta ya kukaangia kiasi
💎Chenga za mkate

JINSI YA KUPIKA
1.Changanya mahitaji  :A: yote mayai yawe ya mwisho kisha, changanya vizuri.

2.Tia vipande vyako vya samaki, halafu wachanganye vizuri waenee viungo kisha
acha kwa dakika 30

3.Chovya kipande kimoja kimoja katika chenga za mkate kisha tia ktk mafuta yaliyokwisha pata moto vizuri,kaanga wakiwa rangi ya brown watoe wachuje mafuta,tayari kwa kula na wali,ugali,chipsi ,chapati n.k.ENJOY!!!

NB;Samaki mwenye mnofu mweupe hupendeza zaidi lakini ukikosa tumia yoyote.

Karibuni....

No comments:

Post a Comment